1
Isaya 43:19
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Muangalie, mimi ninafanya kitu kipya. Kinafanyika sasa hivi, nanyi mutaweza kukiona. Nitafanya njia katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa.
Compare
Explore Isaya 43:19
2
Isaya 43:2
Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.
Explore Isaya 43:2
3
Isaya 43:18
Musiyakumbuke mambo yaliyopita, wala musifikiri juu ya vitu vya zamani.
Explore Isaya 43:18
4
Isaya 43:1
Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.
Explore Isaya 43:1
5
Isaya 43:4
Ninyi ni wa bei kali mbele yangu, ninawaheshimu na kuwapenda. Kwa hiyo, ninatoa watu kusudi niwapate ninyi, ninayaachilia mataifa pahali pa maisha yenu.
Explore Isaya 43:4
6
Isaya 43:3
Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.
Explore Isaya 43:3
7
Isaya 43:5
Musiogope maana mimi nipo pamoja nanyi. Nitawarudisha wazao wenu toka mashariki, nitawakusanya ninyi kutoka magaribi.
Explore Isaya 43:5
8
Isaya 43:25
Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.
Explore Isaya 43:25
9
Isaya 43:10
Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.
Explore Isaya 43:10
10
Isaya 43:11
Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.
Explore Isaya 43:11
11
Isaya 43:13
Mimi ni Mungu na nitakuwa Mungu siku zote. Hakuna anayeweza kuepuka nguvu yangu; hakuna anayeweza kupinga ninayofanya.
Explore Isaya 43:13
12
Isaya 43:20-21
Nyama wa pori wataniheshimu, mbweha na mbuni, maana nitaweka maji katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa, kwa kuwakunywesha watu wangu niliojichagulia, watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, kusudi wazitangaze sifa zangu!
Explore Isaya 43:20-21
13
Isaya 43:6-7
Nitaiambia kaskazini: “Uwaache waondoke”, na kusini: “Usiwazuize! Muwarudishe watu kutoka mbali, kutoka kila pahali katika dunia. Kila mumoja anajulikana kwa jina langu; niliwaumba wote na kuwafanya kwa ajili ya utukufu wangu.”
Explore Isaya 43:6-7
14
Isaya 43:16-17-16-17
Zamani Yawe alifanya barabara katika bahari na kuweka njia kati ya maji mengi. Alipiga kundi la waaskari lenye nguvu, kundi la magari na farasi wa vita, waaskari na mashujaa wa vita. Aliwaangusha chini hata hawawezi kusimama tena, Aliwakomesha na kuwazimisha kama utambi wa taa. Sasa Yawe anasema hivi
Explore Isaya 43:16-17-16-17
15
Isaya 43:15
Mimi ni Yawe, Mutakatifu wenu; Mimi ndiye Muumba wa Israeli, Mufalme wenu.
Explore Isaya 43:15