Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake. Musa akaangalia huku na huko na alipoona kwamba hakuna mutu karibu, akamwua yule Mumisri na kumuficha ndani ya muchanga.