Basi, Musa akainua fimbo yake juu ya inchi ya Misri. Yawe akaleta upepo toka upande wa mashariki, ukavuma juu ya inchi muchana kutwa na usiku kucha. Kulipokucha, ule upepo ukaleta nzige. Wale nzige wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri, wakatua juu ya inchi yote. Nzige wale walikuwa kundi kubwa sana, kiasi ambacho hakijapata kutokea wala hakitatokea tena.