“Kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, yeye atawapa inchi yenye miji mikubwa na mizuri iliyostawi ambayo ninyi hamukuijenga. Nyumba zitakuwa zimejaa vitu vizuri ambavyo ninyi hamukuviweka, kutakuwa visima ambavyo hamukuchimba na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamukuyapanda. Yawe atakapowapeleka kwenye inchi hiyo ambako mutakuwa na chakula chote munachohitaji, muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.