Siku zinakuja ambapo
wakati wa kuvuna utafuata mbio
wakati wa kulima,
wakati wa kukamua zabibu utafuata mbio
wakati wa kupanda mizabibu.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Milima itabubujika divai mupya,
navyo vilima vitatiririka divai.
Nitarudisha hali ya mbele ya watu wangu Waisraeli.
Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi ndani yake;
watapanda mizabibu na kunywa divai yake;
watalima mashamba na kula mazao yake.