Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo. Daudi akatuma mutu kuuliza mwanamuke yule ni nani. Mutu yule akamwambia Daudi: “Mwanamuke yule ni Batiseba binti ya Eliabu, na muke wa Uria wa Hiti.”