Kama ningetaka kujivuna, singekuwa mupumbafu, maana ningesema tu ukweli. Lakini ninaepuka kujivuna, kusudi watu wasinihesabu kuwa mukubwa kuliko vile wanavyoona nikifanya au kunisikia nikisema.
Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.