1
1 Timoteo 4:12
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.
Compare
Explore 1 Timoteo 4:12
2
1 Timoteo 4:8
Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.
Explore 1 Timoteo 4:8
3
1 Timoteo 4:16
Ujiangalie wewe mwenyewe na kuangalia mafundisho yako, nawe ushikamane nayo. Kwa maana ukifanya hivi, utajiokoa wewe mwenyewe na kuokoa wale wanaokusikiliza.
Explore 1 Timoteo 4:16
4
1 Timoteo 4:1
Roho Mutakatifu anasema wazi kwamba katika nyakati za mwisho, watu wengine watapotoka katika imani yao na kufuata roho za udanganyifu na mafundisho ya pepo.
Explore 1 Timoteo 4:1
5
1 Timoteo 4:7
Lakini ukatae hadisi za uongo zilizotungwa na wanawake wazee. Ujizoeze katika maisha yako kumwabudu Mungu kwa ukweli.
Explore 1 Timoteo 4:7
6
1 Timoteo 4:13
Kwa kungojea mpaka nitakapofika, ujitolee kwa kuwasomea watu Maandiko Matakatifu kwa kuwaonya na kuwafundisha.
Explore 1 Timoteo 4:13
Home
Bible
Plans
Videos