1
Wafilipi 4:6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
TKU
Msisumbuke kitu chochote, lakini salini na kumwomba Mungu kwa mahitaji yenu. Mshukuruni Mungu wakati mnapomwomba yale mnayohitaji.
Compare
Explore Wafilipi 4:6
2
Wafilipi 4:7
Na kwa kuwa ninyi ni milki ya Kristo Yesu, amani ya Mungu itailinda mioyo na mawazo yenu isipate wasiwasi. Amani yake inaweza kutenda haya zaidi ya akili za kibinadamu.
Explore Wafilipi 4:7
3
Wafilipi 4:8
Na sasa, mwisho kabisa, kaka na dada zangu, fikirini kuhusu yale yaliyo ya kweli, ya kuheshimiwa, ya haki, yaliyo safi, yenye kupendeza, na yanayosemwa vema.
Explore Wafilipi 4:8
4
Wafilipi 4:13
Kristo ndiye anayenitia nguvu kuyakabili mazingira yote katika maisha.
Explore Wafilipi 4:13
5
Wafilipi 4:4
Furahini katika Bwana daima. Ninasema tena, furahini.
Explore Wafilipi 4:4
6
Wafilipi 4:19
Mungu wangu atatumia utajiri wake wenye utukufu kuwapa ninyi kila kitu mnachohitaji kupitia Kristo Yesu.
Explore Wafilipi 4:19
7
Wafilipi 4:9
Yatendeni yale mliyojifunza na kupokea kutoka kwangu, niliyowaambia na yale mliyoyaona nikitenda. Na Mungu atoaye amani atakuwa pamoja nanyi.
Explore Wafilipi 4:9
8
Wafilipi 4:5
Kila mtu auone wema na uvumilivu wenu. Bwana yu karibu kuja.
Explore Wafilipi 4:5
9
Wafilipi 4:12
Ninajua namna ya kuishi ninapokuwa na vichache na ninapokuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuishi katika hali zote, ninapokuwa na vyakula vingi au ninapokuwa na njaa, ninapokuwa na vingi zaidi ya ninavyohitaji au ninapokuwa sina kitu.
Explore Wafilipi 4:12
10
Wafilipi 4:11
Ninawaambia hili, si kwa sababu ninahitaji msaada kutoka kwa yeyote. Nimejifunza kuridhika na kile nilichonacho na chochote kinachotokea.
Explore Wafilipi 4:11
Home
Bible
Plans
Videos