1
Warumi 10:9
Neno
NEN
Kwa sababu, ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
Compare
Explore Warumi 10:9
2
Warumi 10:10
Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.
Explore Warumi 10:10
3
Warumi 10:17
Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.
Explore Warumi 10:17
4
Warumi 10:11-13
Kama Maandiko yanavyosema, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.” Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na mtu wa Mataifa, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao. Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”
Explore Warumi 10:11-13
5
Warumi 10:15
Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri Habari Njema!”
Explore Warumi 10:15
6
Warumi 10:14
Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?
Explore Warumi 10:14
7
Warumi 10:4
Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kila mtu aaminiye ahesabiwe haki.
Explore Warumi 10:4