Soma Biblia Kila Siku 05/2020预览

Zaburi hii inatukumbusha kwa nini watu wa Mungu wanapaswa wamsifu yeye daima. Ni vema kumwimbia Mungu wetu (m.1) kwa sababu fadhili zake ni zenye upendo, na zi juu ya watu wa Mungu hasa. Pia kwa sababu ya uangalifu wake na wote wenye huzuni na shida, kwa utunzaji wake wa viumbe vyote, na kwa uangalifu wake zaidi kwa wapole na wanyonge. Mungu anafurahi kutoa mahitaji kwa viumbe vyote. Na tusisahau kwamba, Huwaponya waliopondeka moyo, na kuziganga jeraha zao (m.3).