Soma Biblia Kila Siku 01/2025Mfano

Ezra alikuwa mwalimu mwenye ujuzi katika sheria ya aliyokuwa ameitoa BWANA. Pia Ezra alijaliwa na mfalme matakwa yake yote,kama mkono wa BWANA ulivyokuwa pamoja naye(m.6). Akiwa na sifa au vipaji hivi, Ezra alitoka Babeli na kwenda Yerusalemu akiwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza sheria ya BWANA na kuitenda, na kufundisha maagizo na hukumu katika Israeli. Je, wewe katika maisha yako hapa duniani unaitafuta sheria ya BWANA kwa kusomaNeno la Mungu? Unatenda sheria yake, na unamshuhudia Yesu Kristo?
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Januari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko na Ezra. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz