Soma Biblia Kila Siku 01/2025Mfano

Baada ya kurudi kwao kutoka utumwani,Waisraeliwalikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja(m.1). Hii inaonyesha umoja kama watoto wa Mungu. Je, sisi waumini wa Kikristo tunaonyesha umoja au mfarakano? Waisraeli walijenga madhabahuili kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika torati(m.2). Hapa tunaona kuwa pamoja na kukaa uhamishoni miaka mingi, hawakutaka kubadilisha namna ya kuabudu. Je, sisi tunamwabudu Mungu kama anavyotaka yeye, au tumeingiza mambo yasiyompendeza Mungu?
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/2025 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi Januari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Marko na Ezra. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: somabiblia.or.tz