Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku JANUARI/2023Mfano
![Soma Biblia Kila Siku JANUARI/2023](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F34662%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Ushuhuda wa wazi wa Yohana kwamba Yesu ni Mwana Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu, na unyenyekevu wake binafsi kwa Yesu, uliamsha hamu ya wanafunzi wake kumtafuta Yesu. Kama tunavyosoma katika m.37, wale wanafunzi wawili wakamsikia [Yohana] akinena, wakamfuata Yesu. Je, unafahamu waliona nini kwa Yesu hawa wawili? Waliona uzuri uliowafanya wasinyamaze, na hawakunyamaza. Andrea akampeleka Petro, ndugu yake, kwa Yesu. Filipo, jirani yao, naye akamleta Nathanaeli kwa Yesu. Twende kwa Yesu, mimi na wewe. Ameahidi kutufungulia malango ya mbinguni, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya Mwana wa Adamu (m.51).
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku JANUARI/2023](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F34662%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Januari/2023 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma...
More
Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/