Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA SITAMfano

INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA SITA

SIKU 4 YA 7

  

YESU APONYA VIPOFU WAWILI NA BUBU

27 Yesu alipokuwa akiondoka mahali pale, vipofu wawili wakamfuata, wakipiga kelele kwa nguvu na kusema,

“Mwana wa Daudi, tuhurumie!”

28 Alipoingia mle nyumbani wale vipofu wakamjia. Akawauliza,

“Mnaamini kwamba ninaweza kufanya jambo hili?”

Wakamjibu, “Ndiyo, Bwana.”

29 Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema, 

“Iwe kwenu sawasawa na mnavyoamini.”

30-31 Macho yao yakafunguka. Yesu akawaonya vikali, akisema,

“Angalieni mtu ye yote asijue kuhusu jambo hili.”

31 Lakini wao wakaenda na kueneza habari zake katika eneo lile lote.

32 Walipokuwa wanatoka, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu na ambaye hakuweza kuongea aliletwa kwa Yesu.

33 Yule pepo mchafu alipotolewa, yule mtu aliyekuwa bubu akaongea. Ule umati wa watu ukastaajabu na kusema, “Jambo kama hili kamwe halijapata kuonekana katika Israeli.”

34 Lakini Mafarisayo wakasema, 

“Huyo anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa mkuu wa pepo wachafu.”

siku 3siku 5

Kuhusu Mpango huu

INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA SITA

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadi...

More

Tunapenda kushukuru GNPI Afrika kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://gnpi-africa.org

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha