Waroma 12:8-9
Waroma 12:8-9 Biblia Habari Njema (BHN)
Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha. Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
Waroma 12:8-9 Swahili Revised Union Version (SRUV)
mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; msimamizi, na asimamie kwa bidii; anayerehemu, na arehemu kwa furaha. Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkilishika lililo jema.
Waroma 12:8-9 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha. Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.
Waroma 12:8-9 Neno: Bibilia Takatifu 2025 (NENO)
kama ni kutia moyo na atie moyo, kama ni kuchangia kwa ajili ya mahitaji ya wengine na atoe kwa ukarimu, kama ni uongozi na aongoze kwa bidii, kama ni kuhurumia wengine na afanye hivyo kwa furaha. Upendo lazima usiwe na unafiki. Chukieni lililo ovu, shikamaneni na lililo jema.