Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Rum 12

12
Maisha Mapya katika Kristo
1 # Rum 6:11,13; 1 Pet 2:5; Yn 4:24 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 2#Efe 4:23; 5:10,17; Rum 1:28; Gal 1:4Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
3 # 1 Kor 12:11; Efe 4:7 Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani. 4#1 Kor 12:12Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja; 5#1 Kor 12:27; Efe 4:25Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake. 6#1 Kor 12:4-11Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; 7#1 Pet 4:10,11ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; 8#Mt 6:3; 2 Kor 8:2; 9:7mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.
Sifa za Mkristo
9 # 1 Pet 1:22; 1 Tim 1:5; Amo 5:15 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema. 10#2 Pet 1:7; Flp 2:3Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu; 11#Ufu 3:15; Mdo 18:25kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana; 12#1 The 5:17kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; katika kusali, mkidumu; 13#Ebr 13:2kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni mkijitahidi. 14#Mt 5:44; Lk 6:28; Mdo 7:59; 1 Kor 4:12Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani. 15#Zab 35:13Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao. 16#Mit 3:7; Rum 15:5; 11:20Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili. 17#Isa 5:21; 1 The 5:15Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. 18#Mk 9:50; Ebr 12:14Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote. 19#Kum 32:35; Law 19:18; Mt 5:39; 2 The 1:6,7; Rum 13:4; Ebr 10:30Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana. 20#Mit 25:21-22; Mt 5:44Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake. 21Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

Iliyochaguliwa sasa

Rum 12: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha