Hesabu 13:1-2 - Compare All Versions
Hesabu 13:1-2 BHN (Biblia Habari Njema)
Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Tuma watu waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani ambayo ninawapa wana wa Israeli. Utatuma mtu mmoja kutoka katika kila kabila, na mtu huyo lazima awe kiongozi katika kabila lake.”
Hesabu 13:1-2 SRUV (Swahili Revised Union Version)
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila la baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.
Hesabu 13:1-2 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.
Hesabu 13:1-2 NEN (Neno)
BWANA akamwambia Musa, “Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ninayowapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mwanaume aliye mmoja wa viongozi wao.”