Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 120

120
Kuomba msaada
(Wimbo wa Kwenda Juu#120:1 Zaburi hizi huenda ziliimbwa wakati wa kuhiji au kutoka Yerusalemu ambamo kilimani kulikuwa na lile hekalu.)
1Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,
naye akanijibu.
2Uniokoe ee Mwenyezi-Mungu,
na watu wadanganyifu na waongo.
3Enyi watu wadanganyifu, mtapewa kitu gani?
Mtaadhibiwa namna gani?
4Kwa mishale mikali ya askari,
kwa makaa ya moto mkali!
5Ole wangu kwamba naishi kama mgeni huko Mesheki;
naishi kama mgeni katika mahema ya Kedari.#120:5 watu wa Mesheki na Kedari walidhaniwa kuwa wabaya sana.
6Nimeishi muda mrefu mno
kati ya watu wanaochukia amani!
7Wakati ninaposema nataka amani,
wao wanataka tu vita.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 120: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha