Zaburi 114:1-8
Zaburi 114:1-8 BHN
Watu wa Israeli walipotoka Misri, wazawa wa Yakobo walipotoka ugenini, Yuda ikawa maskani ya Mungu, Israeli ikawa milki yake. Bahari iliona hayo ikakimbia; mto Yordani ukaacha kutiririka! Milima ilirukaruka kama kondoo dume; vilima vikaruka kama wanakondoo! Ee bahari, imekuwaje hata ukakimbia? Nawe Yordani, kwa nini ukaacha kutiririka? Enyi milima, mbona mliruka kama kondoo dume? Nanyi vilima, mmerukaje kama wanakondoo? Tetemeka, ee dunia mbele yake Mwenyezi-Mungu; tetemeka mbele ya Mungu wa Yakobo, anayeugusa mwamba ukawa bwawa la maji, nayo majabali yakawa chemchemi za maji!