Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Methali 27:1-4

Methali 27:1-4 BHN

Usijisifie ya kesho, hujui nini kitatokea leo mpaka kesho. Acha watu wengine wakusifu, kuliko mdomo wako wewe mwenyewe. Jiwe ni zito na mchanga kadhalika, lakini usumbufu wa mpumbavu ni mzito zaidi. Ghadhabu ni katili na hasira huangamiza; lakini ni nani awezaye kuukabili wivu?

Soma Methali 27