Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 36

36
Uovu wa watu na wema wa Mungu
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi, mtumishi wa Bwana
1 # Rum 3:18; Mwa 20:11; Mit 8:13; Mhu 12:3 Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake,
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2Kwa maana hujipendekeza machoni pake
Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.
3 # Yer 4:22 Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila,
Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.
4 # Mik 2:1; Isa 65:2 Huwaza maovu kitandani pake,
Hujiweka katika njia mbaya; hauchukii ubaya.
5 # Zab 57:10 Ee BWANA, fadhili zako zafika hata mbinguni,
Uaminifu wako hadi mawinguni.
6 # Ayu 11:8; Rum 11:33; Ayu 7:20; Zab 145:9 Haki yako ni kama milima ya Mungu,
Hukumu zako ni vilindi vikuu,
Ee BWANA, unawalinda wanadamu na wanyama.
7 # Rut 2:12 Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako!
Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.
8 # Ayu 20:17; Ufu 22:1 Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako,
Nawe utawanywesha kutoka mto wa furaha zako.
9 # Isa 12:3; Yer 2:13; Zek 13:1; Yn 4:10,14; Ufu 21:6; Mdo 26:18; Efe 5:8; Kol 1:13; 1 Pet 2:9 Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima,
Katika nuru yako tutaona nuru.
10 # Yer 22:16 Uwadumishie wakujuao fadhili zako,
Na wanyofu wa moyo uaminifu wako.
11Mguu wa kiburi usinikaribie,
Wala mkono wa wasio haki usinifukuze.
12Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu;
Wameangushwa chini wasiweze kusimama.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 36: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha