Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 116:12-19

Zaburi 116:12-19 SRUV

Nimrudishie BWANA nini Kwa ukarimu wake wote alionitendea? Nitakipokea kikombe cha wokovu; Na kulitangaza jina la BWANA; Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA, Naam, mbele ya watu wake wote. Kifo cha waaminifu wa Mungu, kina thamani machoni pa BWANA. Ee BWANA, hakika mimi ni mtumishi wako, Mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako, Umevifungua vifungo vyangu. Nitakutolea dhabihu ya kushukuru; Na kulitangaza jina la BWANA; Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA, Naam, mbele ya watu wake wote. Katika nyua za nyumba ya BWANA, Ndani yako, Ee Yerusalemu.

Soma Zaburi 116