Zaburi 112:1-5
Zaburi 112:1-5 SRUV
Haleluya. Heri mtu yule amchaye BWANA, Apendezwaye sana na maagizo yake. Wazawa wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa. Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yadumu milele. Nuru huwaangaza wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki. Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.