Hesabu 2:1-9
Hesabu 2:1-9 SRUV
BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia, Wana wa Israeli watapanga kila mtu penye bendera yake mwenyewe, na alama za nyumba za baba zao; kuikabili hema ya kukutania ndiko watakakopanga kwa kuizunguka pande zote. Na hao watakaopanga upande wa mashariki, kwa kuelekea maawio ya jua, ndio wale wa bendera ya kambi ya Yuda, kwa majeshi yao; na mkuu wa wana wa Yuda atakuwa Nashoni mwana wa Aminadabu. Na jeshi lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa elfu sabini na nne na mia sita. Na hao watakaopanga karibu naye ni kabila la Isakari; na mkuu wa wana wa Isakari atakuwa Nethaneli mwana wa Suari; na jeshi lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa elfu hamsini na nne na mia nne; na kabila la Zabuloni; na mkuu wa wana wa Zabuloni atakuwa Eliabu mwana wa Heloni; na jeshi lake, na wale waliohesabiwa kwao, walikuwa elfu hamsini na saba na mia nne. Hao wote waliohesabiwa katika kambi ya Yuda walikuwa elfu mia moja themanini na sita na mia nne, kwa makundi yao. Hao ndio watakaotangulia mbele.