Mambo ya Walawi 7:25-27
Mambo ya Walawi 7:25-27 SRUV
Kwani huyo mtu atakayekula mafuta ya mnyama, ambaye ni katika wanyama ambao watu husongeza sadaka kwa BWANA kwa moto, mtu huyo atakayekula mafuta hayo atakatiliwa mbali na watu wake. Tena msiile damu yoyote, ama ya ndege, ama ya mnyama, katika nyumba zenu zote. Mtu yeyote alaye damu, mtu huyo atatupiliwa mbali na watu wake.


