Zab 86:1-4
Zab 86:1-4 SUV
Ee BWANA, utege sikio lako unijibu, Maana mimi ni maskini na mhitaji Unihifadhi nafsi yangu, Maana mimi ni mcha Mungu. Wewe uliye Mungu wangu, Umwokoe mtumishi wako anayekutumaini. Wewe, Bwana, unifadhili, Maana nakulilia Wewe mchana kutwa. Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako, Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana.