Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 23

23
Mchungaji Mwema
Zaburi ya Daudi.
1 # Yn 10:11; 1 Pet 2:25 BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
2 # Ufu 7:17; Eze 34:14 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 # Zab 46:11; Isa 8:10; Zek 8:23; Mt 1:23; Mdo 18:9,10 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
5Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.
6 # 2 Kor 5:1 Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 23: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha