Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 119:41-48

Zab 119:41-48 SUV

Ee BWANA, fadhili zako zinifikie na mimi, Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako. Nami nitamjibu neno anilaumuye, Kwa maana nalitumainia neno lako. Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, Maana nimezingojea hukumu zako. Nami nitaitii sheria yako daima, Naam, milele na milele. Nami nitakwenda panapo nafasi, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako. Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu. Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda. Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako.

Soma Zab 119