Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 119:145-152

Zab 119:145-152 SUV

Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee BWANA, uitike; Nitazishika amri zako. Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako. Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, Naliyangojea maneno yako kwa tumaini. Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku, Ili kuitafakari ahadi yako. Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, Ee BWANA, unihuishe sawasawa na hukumu yako. Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, Wamekwenda mbali na sheria yako. Ee BWANA, Wewe U karibu, Na maagizo yako yote ni kweli. Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.

Soma Zab 119

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha