Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 107:23-32

Zab 107:23-32 SUV

Washukao baharini katika merikebu, Wafanyao kazi yao katika maji mengi, Hao huziona kazi za BWANA, Na maajabu yake vilindini. Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba, Ukayainua juu mawimbi yake. Wapanda mbinguni, watelemka vilindini, Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya. Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi, Akili zao zote zawapotea. Wakamlilia BWANA katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao. Huituliza dhoruba, ikawa shwari, Mawimbi yake yakanyamaza. Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametulia Naye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani. Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu. Na wamtukuze katika kusanyiko la watu, Na wamhimidi katika baraza ya wazee.

Soma Zab 107