Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mit 4

4
Ushauri wa Mzazi
1 # Zab 34:11; Mit 1:8 Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu,
Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.
2Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri;
Msiiache sheria yangu.
3 # 2 Sam 12:24; 1 Nya 29:1 Maana nalikuwa mwana kwa baba yangu,
Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu.
4 # 1 Nya 28:9; Efe 6:4 Naye akanifundisha, akaniambia,
Moyo wako uyahifadhi maneno yangu;
Shika amri zangu ukaishi.
5Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau;
Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu.
6 # 2 The 2:10 Usimwache, naye atakuhifadhi;
Umpende, naye atakulinda.
7 # Mt 13:44; Lk 10:42 Bora hekima, basi jipatie hekima;
Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
8 # 1 Sam 2:30; Dan 12:3 Umtukuze, naye atakukuza;
Atakupatia heshima, ukimkumbatia.
9Atakupa neema kuwa kilemba kichwani;
Na kukukirimia taji ya uzuri.
Maonyo kuhusu Kushika Njia ya Haki
10Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu;
Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
11Nimekufundisha katika njia ya hekima;
Nimekuongoza katika mapito ya unyofu.
12 # Zab 18:36; 91:11; Mit 3:23; 4:19; Yer 13:16; Yn 11:9,10 Uendapo, hatua zako hazitadhiikika,
Wala ukipiga mbio hutajikwaa.
13Mkamate sana elimu, usimwache aende zake;
Mshike, maana yeye ni uzima wako.
14Usiingie katika njia ya waovu,
Wala usitembee katika njia ya wabaya.
15Jiepushe nayo, usipite karibu nayo,
Igeukie mbali, ukaende zako.
16Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara;
Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.
17Maana wao hula mkate wa uovu,
Nao hunywa divai ya jeuri.
18 # Mt 5:14; Flp 2:15; 2 Sam 23:4 Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing’aayo,
Ikizidi kung’aa hata mchana mkamilifu.
19 # 1 Sam 2:9; Ayu 5:14; Isa 59:9,10; Yer 13:16; Yn 12:35 Njia ya waovu ni kama giza;
Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho.
20Mwanangu, sikiliza maneno yangu;
Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu.
21Zisiondoke machoni pako;
Uzihifadhi ndani ya moyo wako.
22Maana ni uhai kwa wale wazipatao,
Na afya ya mwili wao wote.
23Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
24Kinywa cha ukaidi ukitenge nawe,
Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.
25Macho yako yatazame mbele,
Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.
26 # Ebr 12:13 Ulisawazishe pito la mguu wako,
Na njia zako zote zithibitike;
27 # Isa 1:16 Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto;
Ondoa mguu wako maovuni.

Iliyochaguliwa sasa

Mit 4: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha