Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mit 29:10-18

Mit 29:10-18 SUV

Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake. Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza. Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu. Maskini na mdhalimu hukutana pamoja; BWANA huwatia nuru macho yao wote wawili. Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele. Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye. Waovu wakiongezeka, maasi huongezeka; Bali wenye haki watayatazama maanguko yao. Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako. Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.

Soma Mit 29