Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mit 22:7-16

Mit 22:7-16 SUV

Tajiri humtawala maskini, Naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye. Yeye apandaye uovu atavuna msiba, Na fimbo ya ghadhabu yake itakoma. Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake. Mtupe nje mwenye dharau, na ugomvi utatoka; Naam, fitina na fedheha zitakoma. Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo; Mfalme atakuwa rafiki yake. Macho ya BWANA humhifadhi mwenye maarifa; Bali huyapindua maneno ya mtu haini. Mtu mvivu husema, Simba yuko nje; Nitauawa katika njia kuu. Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na BWANA atatumbukia ndani yake. Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali. Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara.

Soma Mit 22