Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayu 14:7-12

Ayu 14:7-12 SUV

Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena, Wala machipukizi yake hayatakoma. Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo; Lakini kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche. Lakini mwanadamu hufa, huifariki dunia; Naam, mwanadamu hutoa roho, naye yupo wapi? Kama vile maji kupwa katika bahari, Na mto kupunguka na kukatika; Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke; Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, Wala kuamshwa usingizini.

Soma Ayu 14