2 Sam 22:21-25
2 Sam 22:21-25 SUV
BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa. Maana nimezishika njia za BWANA, Wala sikumwasi Mungu wangu. Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu; Na kwa habari za amri zake, sikuziacha. Nami nalikuwa mkamilifu kwake, Nikajilinda na uovu wangu. Basi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.