Zaburi 47
47
Zaburi 47
Mtawala mwenye enzi yote
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.
1 Pigeni makofi, enyi mataifa yote,
mpigieni Mungu kelele za shangwe!
2 Jinsi gani alivyo wa kutisha, Bwana Aliye Juu Sana,
Mfalme mkuu juu ya dunia yote!
3 Ametiisha mataifa chini yetu,
watu wengi chini ya miguu yetu.
4 Alituchagulia urithi wetu,
fahari ya Yakobo, aliyempenda.
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Bwana kwa sauti za tarumbeta.
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa,
mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
7 Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote,
mwimbieni zaburi za sifa.
8 Mungu anayatawala mataifa,
Mungu ameketi kwenye kiti chake cha enzi kitakatifu.
9 Wakuu wa mataifa wanakusanyika
kama watu wa Mungu wa Abrahamu,
kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu;
yeye ametukuka sana.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 47: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.