Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 46

46
Zaburi 46
Mungu yuko pamoja nasi
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi.
1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,
msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa,
na milima ianguke kilindini cha bahari,
3 hata maji yake yakinguruma na kuumuka,
na milima itetemeke kwa mawimbi yake.
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu,
mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka,
Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka,
yeye hupaza sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi;
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Njooni mkaone kazi za Bwana
jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia,
anakata upinde na kuvunjavunja mkuki,
anateketeza ngao kwa moto.
10 “Tulieni, mjue kwamba mimi ndimi Mungu;
nitatukuzwa katikati ya mataifa,
nitatukuzwa katika dunia.”
11 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi;
Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 46: NEN

Kuonyesha

Nakili

Linganisha

Shirikisha

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia