Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 135:1-12

Zaburi 135:1-12 NENO

Msifuni BWANA. Lisifuni jina la BWANA, msifuni, enyi watumishi wa BWANA, ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya BWANA, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu. Msifuni BWANA, kwa kuwa BWANA ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza. Kwa maana BWANA amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa hazina yake ya pekee. Ninajua ya kuwa BWANA ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote. BWANA hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote. Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka miali ya radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake. Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama. Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote. Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu: Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani: akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.