Ee BWANA, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako. Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako. Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako. Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako. Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee BWANA, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako. Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako. Ee BWANA, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli. Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
Soma Zaburi 119
Sikiliza Zaburi 119
Shirikisha
linganisha matoleo yote: Zaburi 119:145-152
Hifadhi mistari, soma bila mtandao, tazama klipu za mafunzo, na zaidi!
YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video