Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:145-152

Zaburi 119:145-152 NEN

Ee BWANA, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako. Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako. Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako. Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako. Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee BWANA, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako. Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako. Ee BWANA, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli. Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha