Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 116

116
Zaburi 116
Shukrani kwa kuokolewa kutoka mauti
1Nampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu;
amesikia kilio changu ili anihurumie.
2Kwa sababu amenitegea sikio lake,
nitamwita siku zote za maisha yangu.
3Kamba za mauti zilinizunguka,
vitisho vya Kuzimu#116:3 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, yaani Shimo lisilo na mwisho. vilinipata,
nikalemewa na taabu na huzuni.
4Ndipo nikaliitia jina la Bwana:
“Ee Bwana, niokoe!”
5 Bwana ni mwenye neema na haki,
Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu,
nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7Ee nafsi yangu, tulia tena,
kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8Kwa kuwa wewe, Ee Bwana,
umeniokoa nafsi yangu na mauti,
macho yangu kutokana na machozi,
miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9ili niweze kutembea mbele za Bwana,
katika nchi ya walio hai.
10Nilimwamini Bwana, niliposema,
“Mimi nimeteseka sana.”
11Katika taabu yangu nilisema,
“Wanadamu wote ni waongo.”
12Nimrudishie Bwana nini
kwa wema wake wote alionitendea?
13Nitakiinua kikombe cha wokovu
na kulitangaza jina la Bwana.
14Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana
mbele za watu wake wote.
15Kifo cha watakatifu kina thamani
machoni pa Bwana.
16Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako,
mimi ni mtumishi wako,
mwana wa mjakazi wako#116:16 au mwanao mwaminifu;
umeniweka huru
toka katika minyororo yangu.
17Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru
na kuliita jina la Bwana.
18Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana
mbele za watu wake wote,
19katika nyua za nyumba ya Bwana,
katikati yako, ee Yerusalemu.
Msifuni Bwana.#116:19 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 116: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia