Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 114

114
Zaburi 114
Maajabu ya Mungu wakati Israeli walitoka Misri
1Israeli alipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 114: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia