Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 113

113
Zaburi 113
Kumsifu Bwana kwa wema wake
1Msifuni Bwana.#113:1 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah; pia 113:9.
Enyi watumishi wa Bwana msifuni,
lisifuni jina la Bwana.
2Jina la Bwana na lisifiwe,
sasa na hata milele.
3Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,
jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote,
utukufu wake juu ya mbingu.
5Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu,
Yule aliyeketi kwenye kiti cha enzi huko juu,
6ambaye huinama atazame chini
aone mbingu na nchi?
7Huwainua maskini kutoka mavumbini,
na kuwanyanyua wahitaji
kutoka lundo la majivu,
8huwaketisha pamoja na wakuu,
pamoja na wakuu wa watu wake.
9Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,
akiwa mama watoto mwenye furaha.
Msifuni Bwana.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 113: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia