Mithali 19:13-22
Mithali 19:13-22 NENO
Mwana mpumbavu ni maangamizi ya babaye, naye mke mgomvi ni kama kutonatona kusikoisha. Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa BWANA. Uvivu huleta usingizi mzito, naye mtu mzembe huona njaa. Yeye ambaye hutii mafundisho huulinda uhai wake, bali yeye anayezidharau njia zake atakufa. Yeye amhurumiaye maskini humkopesha BWANA, naye atamtuza kwa aliyotenda. Mkanye mwanao, kwa maana kufanya hivyo kuna tumaini, usiwe mshirika katika mauti yake. Mtu mwenye kukasirika haraka ni lazima atapata adhabu yake, kama utamwokoa, itakubidi kufanya hivyo tena. Sikiliza mashauri na ukubali mafundisho, nawe mwishoni utakuwa na hekima. Kuna mipango mingi ndani ya moyo wa mtu, lakini kusudi la BWANA ndilo litakalosimama. Lile mtu alionealo shauku ni upendo usio na mwisho, afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo.