Mithali 18:7-16
Mithali 18:7-16 NENO
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake. Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu. Mtu aliye mlegevu katika kazi yake ni ndugu na yule anayeharibu. Jina la BWANA ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama. Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa. Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi, bali unyenyekevu hutangulia heshima. Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza, huo ni upumbavu wake na aibu yake. Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili? Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa, masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa. Zawadi humfungulia njia mtoaji, nayo humleta mbele ya wakuu.