Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 13:1-9

Mithali 13:1-9 NENO

Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye, bali mwenye dharau hasikilizi maonyo. Kutoka tunda la midomo yake, mtu hufurahia mambo mema, bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri. Yeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake, bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia. Mvivu hutamani sana na hapati kitu, bali nafsi ya mwenye bidii hutoshelezwa kikamilifu. Mwenye haki huchukia uongo, bali waovu huleta aibu na fedheha. Haki humlinda mtu mwadilifu, bali uovu humwangusha mwenye dhambi. Mtu mmoja hujifanya tajiri, kumbe hana chochote; mwingine hujifanya maskini, kumbe ana utajiri mwingi. Utajiri wa mtu unaweza kukomboa maisha yake, bali mtu maskini hasikii kitisho. Nuru ya mwenye haki hungʼaa sana, bali taa ya mwovu itazimwa.