Mathayo 2:13-15
Mathayo 2:13-15 NENO
Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yusufu katika ndoto akamwambia, “Amka, umchukue mtoto na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko hadi nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.” Kisha Yusufu akaamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri, ambako walikaa hadi Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile neno Bwana alilosema kupitia kwa nabii: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”