YouVersion Logo
Search Icon

Luka 23:50, 51, 52, 53, 54, 55

Luka 23:50 NENO

Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yusufu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi

Luka 23:51 NENO

lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa raia wa Arimathaya huko Yudea, naye alikuwa anaungojea ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.

Luka 23:52 NENO

Yusufu alienda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.

Luka 23:53 NENO

Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.

Luka 23:54 NENO

Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.

Luka 23:55 NENO

Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yusufu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.