Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yeremia 49:1-6

Yeremia 49:1-6 NENO

Kuhusu Waamoni: Hili ndilo asemalo BWANA: “Je, Israeli hana wana? Je, hana warithi? Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi? Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake? Lakini siku zinakuja,” asema BWANA, “nitakapopiga ukelele wa vita dhidi ya Raba, mji wa Waamoni; utakuwa kilima cha magofu, navyo vijiji vinavyouzunguka vitateketezwa kwa moto. Kisha Israeli atawafukuza wale waliomfukuza,” asema BWANA. “Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa! Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba! Vaeni gunia na kuomboleza, kimbieni hapa na pale ndani ya kuta, kwa kuwa Moleki ataenda uhamishoni, yeye pamoja na makuhani na maafisa wake. Kwa nini unajivunia mabonde yako, kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana? Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema, ‘Ni nani atakayenishambulia?’ Nitaleta hofu kuu juu yako kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,” asema Bwana, BWANA wa majeshi. “Kila mmoja wenu ataondolewa, wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi. “Lakini hatimaye, nitarudisha mateka wa Waamoni,” asema BWANA.