Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 24:16-23

Isaya 24:16-23 NENO

Kutoka miisho ya dunia tunasikia uimbaji: “Utukufu kwa Yule Mwenye Haki.” Lakini nilisema, “Ninadhoofika, ninadhoofika! Ole wangu! Watenda hila wanasaliti! Kwa hila watenda hila wanasaliti!” Hofu, shimo na mtego vinakungojea, ewe mtu ukaaye duniani. Kila akimbiaye asikiapo sauti ya hofu atatumbukia shimoni, naye yeyote apandaye kutoka shimoni, atanaswa kwenye mtego. Malango ya gharika ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika. Dunia imepasuka, dunia imechanika, dunia imetikiswa kabisa. Dunia inapepesuka kama mlevi, inayumbayumba kama kibanda kwenye upepo; imelemewa sana na mzigo wa hatia ya uasi wake na ikianguka kamwe haitainuka tena. Katika siku ile BWANA ataadhibu mamlaka zilizo juu mbinguni, na wafalme walio chini duniani. Watakusanywa pamoja kama wafungwa waliofungwa gerezani; watafungiwa gerezani na kuadhibiwa baada ya siku nyingi. Mwezi utatiwa haya, nalo jua litaaibishwa; kwa maana BWANA wa majeshi atatawala juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu, tena mbele ya wazee wake, kwa utukufu.